Monday 5 September 2016

IJUE AMARISON CONSULTANCY


Amarison ni wataalam wa ushauri wa kitaalamu juu ya masuala mbalimbali ya kibiashara.Lengo kuu ni kutoa  ushauri wa kitaalamu utakaomuwezesha mteja wetu kuweza kuiendea biashara yake katika mafanikio ya hali ya juu kwa weledi na ufanisi unaoleta tija.

Ushauri wetu umejikita zaidi katika fani zote za kitaalamu ambazo kwa asilimia kubwa ni hitajio kubwa la kwenye jamii ya mwanadamu.Ushauri unaotolewa huwa ni siri baina yetu na mteja.Kuhifadhi siri ya tunaowahudumia ndio jukumu letu kuu na la msingi.

Katika harakati za maisha ya kila siku binaadamu huwa na shughuli mbalimbali za maendeleo.Shughuli hizo huchangia kwa kiwango kikubwa katika kujenga na kuendeleza taifa.Wakati mwingine mwanaadamu hukwama na kuhitaji ushauri ili kuweza kufanikisha azma yake hiyo.Amarison tupo kwa ajili hiyo.

Kutokana na utafiti tulioufanya tumebaini kuwa kuna aina kuu nne za watu katika jamii katika harakati za kujiletea maendelo.Makundi hayo tunaweza kuyagawa katika muktadha huu:-

1. Watu wenye mawazo ya biashara,

Katika jamii tunayoishi kuna watu wengi sana wana mawazo          mengi ya kibiashara, wana mipango mingi ya kibiashara, ila wamekwama na hawajui wapi na ni kwa vipi waanzie.Hili ni kundi la kwanza ambalo AMARISON tupo kwa ajili yao.Jukumu letu ni kuwaonesha njia ni namna gani wanaweza kuyatoa mawazo yao kutoka katika nadharia na kuyapeleka katika utendaji.

2.Watu waliokata tamaa na maisha

Katika maisha ya mwanadamu kuna mambo mengi sana ambayo humtokea katika maisha ya kila siku na aghalabu wakati mwingine humfikisha mahali mwanadamu hukata tamaa na hata kuona kuna haja ya kuondoka duniani na kuhisi haoni sababu ya kuishi tena kwa namna alivyoharibikiwa au alivyokata tamaa.AMARISON tupo kwa ajili ya watu wa namna hii kwa kuwarejeshea matumaini mapya na kuamsha ari za ndoto zao walizohisi zimekufa na kupiga hatua zaidi.

3. Wafanyabiashara wanaoshindwa kufikia mafanikio 

Katika jamii ya mwanadamu kuna watu hujishughulisha na shughuli za biashara na hushindwa kupiga hatua katika biashara yake kutoka sehemu ya chini kwenda sehemu ya juu zaidi kwa kuongeza au kutanua wigo wa kibiashara na hata wakati mwingine shughuli zake huyumbayumba na hata hufikia mahali hutamani kuachana na biashara zake kwa vile zinavyomuumiza kichwa.AMARISON ipokwa ajili ya kundi hili kuhakikisha wanakuwa na ustawi bora wa kibiashara na kufanya biashara kwa ufanisi wa hali ya juu kuliko hapo awali.

4.Watu wenye rasilimali zote ila waoga wa kuthubutu

Katika jamii ya mwanadamu kuna kundi la watu ambalo hilo lina rasilimali fedha pamoja na nyenzo nyingine za kuendea shughuli za kibiashara lakini wamekuwa waoga sana kiasi cha kuhofia kuwekeza chochote wakifikiria kupata hasara na hela zao kupotoea.Watu hawa wapo ila wamekwama kwa kukosa ujasiri wa kuthubutu.AMARISON ipo kwa ajili ya watu aina hii kwa ajili ya kuwajengea uwezo na kuingia katika shughuli za kibiashara kwa mafanikio na ufanisi.

Amarison ndio suluhisho lako hujachelewa anza sasa.
wasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu hapo juu.
Ahsante.

2 comments:

  1. Hello !
    Welcome to the "Directory Blogspot"
    We are pleased to accept your blog in the division: TANZANIA
    with the number: 63
    We hope that you will know our website from you friends,
    Invite your friends by giving them the "Directory award"
    This is the only way to expand the site.
    The activity is only friendly
    Important! Remember to follow our blog. thank you
    Have a great day
    friendly
    Chris
    For other bloggers who read this text come-register
    http://world-directory-sweetmelody.blogspot.com/
    Imperative to follow our blog to validate your registration
    Thank you for your understanding
    ++++
    Get a special price "Directory award" for your blog! with compliments
    Best Regards
    Chris
    A pleasure to offer you a degree for your site
    http://nsm08.casimages.com/img/2015/04/22//15042212171618874513195366.png

    ReplyDelete
  2. http://world-directory-sweetmelody.blogspot.fr/search/label/Africa%20Tanzania___________63%20Members

    ReplyDelete