Friday 24 March 2017

CONSULTATION BUSINESS ndio mpango mzima 1:

Awali ya yote nimshukuru Mwenyezimungu kwa kunijaalia afya njema na kuweza kuandika haya.


Kumekuwa na kelele nyingi sana juu ya waimbi la vijana waliohitimu kuwa hawajaajiriwa na hawana ajira wengi wao. Siwezi kulaumu maana mfumo wa elimu ya juu vyuoni mwetu umewekeza zaidi katika kusomesha watu waweze kuajiriwa kuliko kujiajiri.


Suala la ajira ni mtambuka bali kuamua kuingia katika ajira ya aina gani baada ya kuhitimu masomo ni uamuzi wako mwenyewe.Wapo wengi wamesoma shahada mbalimbali ila leo wameziweka kando kwa muda wakiwa wamewekez akwenye mambo mengine kabisa ili mradi tu atumie ujuzi mpya katika kukabili changamoto za kimaisha kwa kuweza kuzalisha kipato na maisha yazendelee.


Kusoma ni jambo moja kuwa na ajira ni jambo la pili unapomaliza masomo yako jitahidi saana ujifunze ujuzi ambao unapatikana mtaani ili uweze kuzibaini fursa na kuzitumia kuweza kujiajiri.


Kijana msomi anafursa kubwa sana ya kuwa CONSULTANT yaani mtu anayetoa ushauri wa kitaalamu unaohitajiwa kusaidia kutatua changamoto za watu kwa kuwa anayo elimu tayari ni kiasi cha kupata semina ya namna gani atautumia ujuzi wake aweze kujiajiri.


Kama umehitimu chukua trasctipt yako yaani matokeo yako kisha jaribu kuipitia uone juu ya kozi zote ulizosoma kisha jiulize kwa sasa mtaani kuna kozi gani inanihitaji na kama nikiamua kuitumia nabadilisha maisha?


Ukishajiuliza swali hili jua hutakosa cha kufanya kulingana na ujuzi ulionao.Usiingalie shahada yako angalia kozi ulizosoma zenye kuunda shahada yako utagundua una mambo mengi unayoyajua ila kuna moja ni muhimu sana mtaani hili litakusaidia kubaidli maisha yako kama utaamua kulitumia.


Uwekezaji katika taaluma ya kutoa ushauri wa kitaalamu kwanza inahitaji sana uzoefu wa hali ya juu ambao kwa wakati husika utakuwa huna hivyo sasa utatakiwa kuanza katika hatua za awali mambo mengi kwako yatakuwa ya kujitolea ili baadae uweze kupata uzoefu na kuwa na jina la kibiashara.


Wengi wetu hatupendi kujitolea kufanya kazi  kwenye makampuni mbalimbali kumbuka unapoamua kujitolea ndio unajifunza ujuzi husika kwenye kampuni husika ujuzi huu unakujeng ana kukufanya uje kuwa mtaalam hapo baadae.


Maisha ya kutoa ushauri wa kitaalamu huanza na kufanya kazi nyingi za kujitolea wakati mwingine huwa ni kazi tofauti ili hizi zote hukujenga na kuwa mtaalamu hapo baadae .Anza na kujitolea kwa kutumia ujuzi na elimu yako kisha hapo baadae utaweza tu kufanikiwa kujiajiri.


Kozi zote chuo ulizosoma ni muhimu kama utazitafsiiri kivitendo zibadili maisha yako .


Itaendelea...........

No comments:

Post a Comment