Friday 24 March 2017

CONSULTATION BUSINESS ndio mpango mzima 1:

Awali ya yote nimshukuru Mwenyezimungu kwa kunijaalia afya njema na kuweza kuandika haya.


Kumekuwa na kelele nyingi sana juu ya waimbi la vijana waliohitimu kuwa hawajaajiriwa na hawana ajira wengi wao. Siwezi kulaumu maana mfumo wa elimu ya juu vyuoni mwetu umewekeza zaidi katika kusomesha watu waweze kuajiriwa kuliko kujiajiri.


Suala la ajira ni mtambuka bali kuamua kuingia katika ajira ya aina gani baada ya kuhitimu masomo ni uamuzi wako mwenyewe.Wapo wengi wamesoma shahada mbalimbali ila leo wameziweka kando kwa muda wakiwa wamewekez akwenye mambo mengine kabisa ili mradi tu atumie ujuzi mpya katika kukabili changamoto za kimaisha kwa kuweza kuzalisha kipato na maisha yazendelee.


Kusoma ni jambo moja kuwa na ajira ni jambo la pili unapomaliza masomo yako jitahidi saana ujifunze ujuzi ambao unapatikana mtaani ili uweze kuzibaini fursa na kuzitumia kuweza kujiajiri.


Kijana msomi anafursa kubwa sana ya kuwa CONSULTANT yaani mtu anayetoa ushauri wa kitaalamu unaohitajiwa kusaidia kutatua changamoto za watu kwa kuwa anayo elimu tayari ni kiasi cha kupata semina ya namna gani atautumia ujuzi wake aweze kujiajiri.


Kama umehitimu chukua trasctipt yako yaani matokeo yako kisha jaribu kuipitia uone juu ya kozi zote ulizosoma kisha jiulize kwa sasa mtaani kuna kozi gani inanihitaji na kama nikiamua kuitumia nabadilisha maisha?


Ukishajiuliza swali hili jua hutakosa cha kufanya kulingana na ujuzi ulionao.Usiingalie shahada yako angalia kozi ulizosoma zenye kuunda shahada yako utagundua una mambo mengi unayoyajua ila kuna moja ni muhimu sana mtaani hili litakusaidia kubaidli maisha yako kama utaamua kulitumia.


Uwekezaji katika taaluma ya kutoa ushauri wa kitaalamu kwanza inahitaji sana uzoefu wa hali ya juu ambao kwa wakati husika utakuwa huna hivyo sasa utatakiwa kuanza katika hatua za awali mambo mengi kwako yatakuwa ya kujitolea ili baadae uweze kupata uzoefu na kuwa na jina la kibiashara.


Wengi wetu hatupendi kujitolea kufanya kazi  kwenye makampuni mbalimbali kumbuka unapoamua kujitolea ndio unajifunza ujuzi husika kwenye kampuni husika ujuzi huu unakujeng ana kukufanya uje kuwa mtaalam hapo baadae.


Maisha ya kutoa ushauri wa kitaalamu huanza na kufanya kazi nyingi za kujitolea wakati mwingine huwa ni kazi tofauti ili hizi zote hukujenga na kuwa mtaalamu hapo baadae .Anza na kujitolea kwa kutumia ujuzi na elimu yako kisha hapo baadae utaweza tu kufanikiwa kujiajiri.


Kozi zote chuo ulizosoma ni muhimu kama utazitafsiiri kivitendo zibadili maisha yako .


Itaendelea...........

Saturday 11 March 2017

TANGA NA FURSA YA UWEKEZAJI

Mkoa wa Tanga ni mkoa uliosheheni kila aina ya fursa ya kiuchumi kutokana na miundombinu yake inayopelekea maeneo mengi kufikika kwa urahisi.Pia mkoa huu unapakana na nchi jirani ya Kenya kupitia mji wa Mombasa unaoifanya Tanga izidi kuwa sehemu nzuri ya kuwekeza na hata kusafirisha bidhaa mbalimbali nchi jirani na kujipatia fedha za kigeni.

Mkoa wa Tanga umejaaliwa kuwa na bahari ya hindi ambayo ni fursa nyingine ya kusafirisha bidhaa mbalimbali nje ya nchi hususan nje ya Afrika Mashariki.Uwepo wa bahari ni neema kubwa kwa watu wa Tanga na uchumi wa mji huu.Bahari huwezesha meli kusafirisha mizigo na bidhaa mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Iwapo uchumi wa bandari utakuzwa kwa kiwango cha hali ya juu na kuwa na bandari ya kubwa na ya kisasa milango ya uchumi wa Tanga itazidi kufunguka maana itakuwa ni kiunganishi kikubwa hata na nchi za Ulaya na za Asia.

Nchi nyingi duniani zilizokuwa na bahari na kuamua kuwekeza kwenye uchumi wa bandari hakika zimewafugulia milango katika kukuza sekta ya uchumi wa viwanda na hata biashara pamoja na sekta ya utalii.

Hapo awali mji wa Tanga ulisifika sana kwa uchumi unaoliendesha Taifa la Tanzania hususan kwenye sekta ya kilimo cha mkonge na korosho halikadhalika katika upande wa viwanda mji wa Tanga ndio ulikuwa gwiji katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo nguo,usindikaji wa matunda ,maziwa,chuma,saruji,bidhaa za viuongo mbalimbali.Kiukweli ukielezea historia ya mji wa Tanga kiuchumi unaweza kutoka machozi maaana yale yote yaliyoiletea sifa Tanga na Tanzania ndani ya mji wa Tanga leo yamekuwa ni magofu na magereji na hali ya uchumi wa viwanda umekuwa kizungumkuti.Hakuna mtanzania asiyeijua Tanga na uchumi wake ulivyokuwa ukiiendesha Tanzania.

Hiyo ni historia haina maana historia iachwe ipite tu lahasha historia pia hutukumbusha kuwa inatabaia ya kujirudia.Sasa ni zemu yetu Tanga kuchanua kwa uchumi wa bandari viwanda na biashara.

Iwapo wana Tanga wenyewe hawataamka na kuhamasisha juu ya fursa za uwekezaji zilizoko ndani ya mji wa Tanga wawekezaji wengi katika sekta mbalimbali watavutika na kuja kuwekeza.Kuna uwezekano mkubwa tu wapo wanaotaka kuwekeza Tanga bali hudanganywa au hata kutishwa na baadhi ya watu tu eti Tanga hakuna mzunguko wa hela utapata taabu.Dhana hizi haziwezi kubadilishwa kama wana Tanga tutakaa kimya juu ya Tanga yetu.

Zamu yetu sasa kuirejesha heshima na hadhi ya Tanga makampuni mbalimbali yameonesha nia na dhamira ya kuja kuwekeza Tanga wakati ndio huu wa kupambana kutangaza fursa zote zile za uwekezaji ndani ya mji wa Tanga na wilaya zake.

Tanga ni zaidi ya dhahabu lulu au almasi ina neema za kila aina na utajiri mkubwa wa rasilimali za kila aina wakati ndio huu tuhamasishane kuwekeza ndani ya Tanga kwa kuzielezea fursa mbalimbali za uchumi ndani ya mkoa wa Tanga.

AMARISON CONSULTANCY tumeanza kuitangaza TANGA NA FURSA ZA UWEKEZAJI na wewe tumia fursa yako kuitangaza TANGA.

TANGA KWANZA

Usikose toleo lijalo tutaanza na WILAYA YA MKINGA NA FURSA YA UWEKEZAJI

Thursday 20 October 2016

MIKOPO ELIMU YA JUU

Nawashangaa watanzania

MTU anasomesha mtoto ada milioni 3

Analalamika kukosa mkopo wa 1.5 m kulipia ada ya chuo kwa MWAKA

Watu wanailaumu serikali eti wanafunzi wamekosa mikopo bali hawalaumu waliokopeshwa kuingia mitini kutokulipa

Wanasingizia hawana ajira wakati kuna kujiajiri na kwa mwezi unatakiwa kulipa kima cha 50000 kwenda juu hiki ni kiwango nilichokuwa nikilipa deni langu la bodi ya mikopo sijui sasa kima cha chini ni kiasi gani.

Hukusoma ili uajiriwe umesoma ili uondoe ujinga na upumbavu hatimaye ujiajiri.  uendeshe maisha yako na ulipe deni la mkopo wa elimu ya juu.

Ni ujinga wa hali ya juu kusema wanafunzi 66000 wa elimu ya juu wamekosa mikopo

Wakati kuna vijana zaidi ya milioni toka 1994 mpaka 2015 hawajalipa hata shilingi wanadaiwa .

ILI WATANZANIA WENGINE WAWEZE KUKOPESHWA KUSOMA ELIMU YA JUU

WEWE ULIYEMALIZA MWAKA 1994 HADI 2015 LIPA ILI WENGINE WAKOPESHWE.

Kwanza jamii yetu ishajitenga siku nyingi eti wanaosoma shule za serikali ni masikini na wanaosoma shule za kulipia ni matajiri.

Katika msingi huu wanaomaliza Shule za serikali nashauri wapewe kipaumbele kwenye mikopo maana hawana uwezo.

Serikali na bodi ya mikopo nashauri kigezo kimojawapo cha kupata mkopo wa elimu ya juu iwe ni kuangalia anayeomba amehitimu elimu Yake Wapi

Shule ya msingi

Shule ya sekondari

Kidato cha sita

Maaana kuna wanaolipa milioni 4 kusomesha  chekechea eti na wao wapewe mikopo kwa kuwa wana watoto elimu ya juu alaaaa

Dahh ningekuwa nina mamlaka ya mwisho

Ningehakikisha aliyesoma Shule ya msingi ya serikali la kwanza hadi la saba pamoja na sekondari ya serikali na kidato cha sita kahitimu Shule ya serikali hakika huyu angepata mkopo 100%

Hapa hakuna ubaguzi maana wakati wewe unasoma Shule ya mamilioni na mwingine anasoma shule ya elimu bure hukuuona huo ubaguzi ndio uje kuuona chuo kikuu kwa kuwa umekosa mkopo?

Kama uliweza kulipa malaki na mamilioni kuanzia shule ya msingi endeleaaa tu baba kulipa mamilioni elimu ya juu iweje ule ng'ombe mzima uahindwe mkia?

Kama kuna aliyesoma kwa ada ya chini ya laki moja elimu ya msingi mpaka kidato cha sita aendelee tu kusaidiwa na serikali kukopeshwa na kupata elimu ya juu maana huyu ndio hana uwezo.

KILA MBUZI ATAKULA KWA UREFU WA KAMBA YAKE.

Amarison
2016

Monday 10 October 2016

TUMIA WAYA ZA MASTER CABLE KWA USALAMA WA JENGO LAKO

MASTER CABLE ni waya za umeme zenye kiwango na ubora wa hali ya juu uliotihibitishwa na TBS

Waya za MASTER CABLE zinatengenezwa nchini TANZANIA

Copper halisi yenye kiwango na ubora wa hali ya juu ndio inayotumika kutengeneza waya za MASTERCABLE

Ubora wa waya za MASTER CABLE umepimwa kwa kuzingatia viwango vyote vya ubora.

WAYA za MASTERCABLE zinapimwa katika uwezo wa kubeba mkondo wa umeme 3000VOLT ambapo umeme wa kawaida kwa matumizi ya kitanzania ni 250 volt .

Hiki ni kiwango bora kabisa cha kupima ubora wa WAYA DUNIANI katika kuhimili mkondo wa umeme hii inakuhakikishia kuwa hata kama umeme utazidi kwa ghafla hauna uwezo wa kuleta madhara ndani ya nyumba yako maana WAYA ZA MASTER CABLE zinauwezo mkubwa wa kuhimili mkondo wa umeme hata ule usio wa hali ya kawaida.

Tafadhali kwa USALAMA WA JENGO lako TUMIA WAYA ZA MASTER CABLE

Waya zetu ni

1.5 single

2.5 single

1.5 twin

2.5 twin

4 twin

6 twin

Waya za single kuna za red green na black

Plastic inayotumika kufunika waya yaani PVC kwa wale wasiofahamu ile ngozi ya juu ya waya ina ubora wa hali ya juu ambayo ina uwezo wa kuhimili joto kubwa sana bila kupata madhara.

PVC hujaribiwa kupitia kifaa maalum ambapo waya huingizwa katika kifaa hicho kikiwa na maji ya moto yenye nyuzi joto 70 na kupewa volt ya umeme 3000 kwa kuzingatia joto la maji na joto la mkondo wa umeme ndipo uimara wa PVC huthibitika. Hapa tunapima uwezo wa PVC kuhimili joto na kutokulainika .

Kwa kuzingatia haya ndipo tunathubutu kusema WAYA ZETU NI BORA NA ZINA KIWANGO KILICHOTHIBITISHWA NA TBS waya zetu ije jua ije mvua haziwezi kuleta madhara katika NYUMBA yako.

MASTER CABLE

"We are the master of cables in Tanzania"

Waya zetu zinapatikana katika maduka yote yenye vifaa vya umeme kariakoo DSM

Usinunue waya nunua MASTER CABLE

Bei za waya zetu utazipata madukani maduka ya jumla na rejareja kwa sasa waya zipo MADUKA YOTE KARIAKOO DSM na ARUSHA .

Kwanini uhatarishe usalama wa NYUMBA yako kwa kutumia waya zisizobora?

Waya zetu zote zipo katika ujazo wa 100m kwanini ununue waya pungufu wakati waya bora zipo?

Waya zetu za twin zina poda inayoimarisha na kuupa waya wetu kiwango cha kimataifa zaidi.

Usihangaike na bidhaa fake nunua waya wenye ubora.







BEI ZA WAYA ZETU NI KWASABABU YA UBORA WETU

Wakati ni huu sasa TUMIA MASTERCABLE KWA USALAMA WA JENGO LAKO

Wakati ni huu

TUMIA MASTERCABLE KWA USALAMA WA JENGO LAKO

KUTOKUWA NA AJIRA NI TATIZO LA" MTAZAMO POFU"


Mtazamo pofu ni aina ya mtazamo ambao mtu anakuwa hana uwezo wa kuona jambo zaidi ya upeo wake wa ziada bali huweza kuliona jambo katika mtazamo mmoja tu.

Jamii na kila mwanajamii analalamika kuwa hana ajira.Kilio hiki ni kikubwa sana kwa vijana wasomi kwasababu wao wanaamini zaidi juu ya ajira ya kuajiriwa na si kujiajiri.

Iwapo utawahoji na kujadiliana nao juu ya ajira ya kujiajiri basi jambo moja kuu litakalokuwa kikwazo kwa vijana wasomi watakwambia hawana mtaji.Wakimaanisha mamilioni ya hela ya kuweza kufanya biashara.

Mtazamo pofu huanzia pale mtu anapoitazama ajira kuwa ni lazima uwe umeajiriwa sehemu fulani uko kwenye kiti cha kuzunguka una nesanesa na kupulizwa na kiyoyozi ila hana imani juu ya ajira ya kujiajiri.

Mtazamo pofu pia hujitokeza pale unapotazama mtaji kuwa ni hela ya kuanzia biashara huu nao ni mtazamo pofu maana umeshindwa kuweza kuona yaliyokuwepo zaidi ya hapo.

Angalia maisha ya vijana waliohitimu vyuo vikuu wanavyohangaika kutafuta kazi huku wakiwa tayari kichwani wana maarifa yenye nadharia nyingi na mipango mingi ya mafanikio ila wameshindwa kuamua kutekeleza kivitendo maarifa hayo ili yawapatie kipato.

Tazama vijana walioishia kidato cha 4 au cha 6 wako mtaani wakifanya biashara zao na wanaendesha maisha yao kwa ufanisi tu,  msomi ana hahaha mtaani kutafuta kazi huu ndio upofu.

Niliamua kuchukua muda katika maisha yangu kuanza kulifanyia utafiti haswa kwa hawa vijana ambao wao hawakufikia elimu ya juu ila  wengi wao ndio wafanyabiashara na ni wajasiriamali huku wasomi wakibaikia katika hatua ya kuajiriwa na hao na kulia njaa kila baada ya siku.

Kitu nilichokibaini ni kuwa, vijana hawa ambao hawakufika elimu ya juu wao wana uthubutu ujasiri subra na uvumilivu saana katika kuyaendea maisha yao na wana nidhamu kubwa ya matumizi ya pesa kwasababu wanajua ugumu wake na kupatikana kwake kwa namna wanavyoitafuta katika biashara zao za kila siku.

Kitu kingine ambacho nimekigundua kutoka kwa vijana ambao ni wafanyabiashara na hawakufikia elimu ya juu kuwa wao wanaishi maisha yao halisi si maisha ya kutaka kuonekana kuwa ni watu wa hali flani ya juu kimaisha ambapo matumizi yao yamekuwa ni ya wastani na muda mwingi hufikiria zaidi kuwekeza katika fursa nyingine za kibiashara.

Jambo la mwisho nililolibaini ni kuwa wao kila fursa wanaiona ni njia ya kuitumia kujipatia kipato cha halali.Nilipojaribu kuwahoji na kuuliza asilimia kubwa kati yao wakati nikiwauliza mwanzo wa biashara zao walinijibu uaminifu ndio mtaji wake alioanza nao ambapo mpaka leo analetewa mizigo anauza na kulipa kama kawaida.

Wakati msomi akihangaika na business plan na maandiko mradi kutafuta wadhamini na wahisani huku akiamini juu ya mtaji pesa tayari kuna ambao wao wameanza na mtaji uaminifu.

Yupo aliyenisimulia maisha yake kuwa yeye aliamua kuchukua bidhaa kwa mtu na kuanza kusambaza katika maduka na katika kila bidhaa aliyokuwa akisambaza yeye alikuwa akiongeza shilingi 1000 au 500 ambapo leo hii ana miliki duka kubwa sana la simu na vipodozi katikati ya jiji la Dar es salaam.

Kila ukimuuuliza jibu atakwambia kaka mimi sijasoma nimeishia kidato cha 4 ila uaminifu ndio umenifanya nimefika hapa.Hakika ukisikiliza historia zao watu hawa unaiona tofauti kubwa sana kati ya kijana msomi na kijana aliyeishia kidato cha nne katika uthubutu wa kujaribu na kujiajiri.

Duniani kote inaonesha dhahiri kuwa sekta ya ajira ya kuajiriwa iwe ni serikalini au sekta binafsi ni 25% tu kila mwaka wanaoajiriwa kutoka kwa waliohitimu katika kila nchi katika sekta zote.Je 75% inakwenda wapi? Hapa ndipo unapoiona sekta ya kilimo na ufugaji ikisubiri 75% sekta ya uvuvi ikisubiri 75% sekta ya ujasiriamali  na uchuuzi ikisubiri asilimia iliyobaikia.

Katika mazingira haya ndipo unapoona mtazamo pofu wa kuiona ajira ya kuajiriwa na kutokuiona ajira ya kujiajiri hatimaye kila msomi huililia serikali kutoa ajira.

JUKUMU LA SERIKALI dunia nzima ni kujenga miundombinu bora na imara ya raia wake kuweza kupata maarifa yaani elimu itakayowawezesha wao kuzikabili changamoto zilizopo katika mazingira yao na sio kuajiriwa.Ikiwa umehitimu shahada ya kwanza na mpaka leo unahangaika kutafuta ajira na huzioni fursa za wewe kujiajiri basi jua pamoja na elimu yako na wewe una mtazamo pofu.

Duniani hakuna serikali inayoajiri 100% katika 25% hugawana na sekta binafsi sasa wewe unayesubiria kuajiriwa utasubiri sana maana wapo wengi kama wewe wanaendelea kulia na kusota mtaani wamebakia kujisifu kuwa wamesoma sana.Wamebaikia na vyeti wakiviangalia kama picha na kuvisoma kama magazeti.

Acha kujidanganya na hivyo vyeti sekta ya kujiajiri haingalii mivyeti yako inaangalia upeo na akili yako ya kuweza kuyaona maisha nje ya mtazamo wa darasani ulipokuwa ukisoma.

Ukitaka kujiajiri sahau kwa mda habari za degree yako huku mtaani kwenye kujiajiri hiyo haina nafasi kwa mwanzo utakuja kuitumia mbeleni.Ile elimu uliyoipata ambayo ipo kichwani kwako ndio sasa inatakiwa ikuoneshe namna gani unaweza kuziona fursa na kuziendea.

kumbuka : HUSOMI ILI UAJIRIWE UNASOMA KUFUTA UJINGA NA UPUMBAVU ili uweze kupata maarifa yatakayokuwezesha kukupa mbinu bora ya kuzikabili changamoto za maisha yako.

KAMA ULISOMA KWA MTAZAMO HUU WA KUAJIRIWA UJUE UNA MTAZAMO POFU

Makala hii ni kwa ajili ya wewe ambaye mpaka leo unasubiri kuajriwa.

NINI CHA KUFANYA kuondokana na mtazamo huu pofu endelea kufuatilia

www.amarisontanga.blogspot.com 

kwa elimu zaidi.

Wednesday 28 September 2016

TANGA NA UTALII

TANGA NA FURSA YA UTALII

Katika sekta ya utalii ni kama vile mji wa Tanga umesahaulika katika nchi ya Tanzania.Wengi wakielezea hutalii huelezea zaidi juu ya mbuga za wanyama na haswa hicho ndio kimefanywa kuwa ndio kivutio kikubwa cha utalii au uwepo wa mambo ya kale.Jambo hili ni upotofu wa hali ya juu.

Suala la utalii ni pana mno na utalii umegawika katika makundi anuai :

Utalii wa uwanda wa ardhi:Hii ni aina ya utalii ambapo watalii huajabia namna umbile la ardhi la sehemu fulani lilivyo mfano uwepo wa ardhi tambarare yenye nyasi ndogondogo au uwepo wa ardhi tambarare yenye changarawe ambayo imeenea eneo kubwa au uwepo wa milima mambonde makubwa yenye kustaajabisha ni vivutio vya utalii.

Tanga kwa hili tuna milima ya usambara ambayo INA jiografia kubwa na ya kuvutia Juhudi za kuitangaza LUSHOTO na AMANI katika kivutio hiki bado iko chini sana kiasi cha kuifanya TANGA kuonekana kama vile suala la utalii halina nafasi.

Utalii wa mito: Maporomoko ya maji kutoka katika maeneo ya juu ya mito ni kivutio kikubwa sana katika sekta ya utalii.Hili huonekana kama vile halina nafasi Tanga na kuonekana kama vile hakuna mito mikubwa na yenye maporomoko ya kustaajabisha kumbe Tanga tuna mto zigi ambao ndio tegemeo la maji ya kutumia katika jiji la Tanga mto huu hutokea juu kabisa kwenye milima ya usambara ambapo chemchem yake ndipo ilipoanzia.

Tuna mto Pangani ambao huu nao una mchango mkubwa katika kuzalisha umeme wa Taifa hili MTO huu mlango wake wa kuingilia bahari ya hindi hukutana na bahari na hakika maji ya mto huu hayachanganyiki na maji ya bahari.

Wangapi washalitangaza hili wangapi washalifanyia utafiti hili na kutangaza kivutio hiki cha utalii?

Maporomoko ya maji yaliyopo milima ya usambara nani ameyatangaza? Kituo cha kuzalisha umeme wa maji cha Pangani kilichopo Hale je ni nani amekitangaza? Kwa kawaida sekta ya utalii hukua katika eneo husika kulingana na namna wana jamii wanaoishi katika eneo husika wanavyoutangaza utalii wa kwao.Tusione maeneo yenye mbuga za wanyama kuwa ni kivutio kikubwa cha utalii ni kwasababu wenyeji wa maeneo hayo waliamua kuutangaza utalii huo na kuufanya kuwa ni sehemu ya ajira na kuwaingizia kipato.

Utalii wa bahari : Mungu katujaalia kuwa na fukwe kubwa sana lakini mpaka sasa utalii wa bahari bado haujajulikana na kutangazwa .Utalii wa bahari kuna visiwa vingi ndani ya bahari ya Hindi ukanda wa Tanga Tanga ambavyo vina historia kubwa na maajabu mengi sana mfano KISIWA MWEWE pwani ya MOA, KISIWA CHA MTANG'ATA PWANI YA TANGA,KISIWA CHA FUNGUNI PWANI YA TANGA  kama hatutaamua kuitangaza Tanga yetu na utalii hakuna atakayekuja kututangazia.

Utamaduni wa uvuvi na namna ya kuvua ni sehemu mojawapo ya utalii wa bahari ukanda wa Tanga una utamaduni wa asili katika kuvua ambapo ukiwaona wavuvi wakiitekeleza shughuli hii kwa tamaduni zao huwa ni yenye kuvutia .Nani atautangaza utalii wa Tanga kama sio mimi na wewe.? Migodi ya utengenezaji chumvi kilimo cha mwani hivi vyote ni vivutio vya utalii wa bahari.Fukwe ambazo tunazo ndani ya Mkoa huu wa Tanga zenye mandhar nzuri na za kuvutia lakini je zimetangazwaje? Tunashuhudia watu husafiri kuajabia ziwa Victoria lakini huwaoni kusafiri kuajabia maajabu ya bahari ya hindi katika upwa huu wa Tanga.Hii ni kwasababu hatujaamua kuifanya Tanga kuwa ni sehemu ya utalii.

Utalii ni tasnia inayotengenezwa,haitoshi tu kuwa na mazingira asilia bali ni kwa kiwango gani mazingira hayo yametengenezwa kuwa kivutio cha utalii?

Angalia utalii wa bahari unavyotengenezwa

Moja ,uwepo wa fukwe , ni lazima pia kuwepo na vifaa vya michezo na michezo inayoambatana na utalii wa fukwe kama viwanja vya michezo kandokando ya fukwe.Viwanja hivi huwa na mazingira yaleyale ya asili na hufuata kanuni zote za uhifadhi wa mazingira ya fukwe.

Pili, vifaa vya kuchezea majini kama ngalawa boya hizi ni ngalawa maalum ambazo hutumiwa kuchezea michezo ya ndani ya maji kwa kuyakata mawimbi.

Tatu, uwepo wa hotel nzuri za kisasa na zenye mandhari ya pwani zinazozingatia gharama kwa mtuvwa ndani na mgeni kutoka nchi nyingine.MFANO tunaona TICC MCHUKUUNI wamejaribu kufanya kitu cha namna hii na wageni huja wengi tu kuajabia mazingira ya bahari.

Bwawa la viumbe vya baharini, ni lazima kuwe na bwawa kubwa sana lililojengwa katika mandharu ya kuvutia ambapo linaweza kumsaidia mtu kuona kila aina ya samaki waliomo baharini na maisha yao kwa ujumla.Katika kulindeleza hili baadhi ya nchi wamejenga hotel ambazo ukiingia unaiona sehemu ya maji ya bahari na viumbe mbalimbali hili nalo ni sehemu mojawapo kubwa ya utalii wa bahari.Dubai katika utalii wa bahari wamefanikiwa mno.

Utalii wa mambo ya kale na utamaduni wa eneo husika.Tanga INA historia kubwa sana ndani ya nchi hii ya Tanzania lakini kwa kutoelezwa historian hiyo katika muktadha wa utalii ni kama vile imevizwa.Tuna makaburi ya wajerumani,Waingereza nakadhalika haya yakuelezwa katika muktadha wa utalii tayari tosha huwa ni kivutio cha utalii sisi ni matajiri w mambo ya kale lakini tumejidharau kwenye hili hakuna atakayetujua.Angalia mathalani Shule ya kwanza ya msingi Tanzania wakati huo Tanganyika ni Magila Shule ya kwanza ya sekondari ni Old Tanga nani kaziwekea sura ya utalii vitu hivi? Manispaa ya kwanza Tanganyika au Deutch Osta Afrika ilikuwa ni Tanga Nani kaiwekea sura ya utalii ?

Tuna kuta kubwa sana maeneo ya vijiji vingi vya pwani mathalani moa lakini je ni Nani kazielezea kuta au ngome hizi zilikuwa ni za nini?

Je waijua mashine ya kusaga unayotumia nguvu ya maji ambayo ilijengwa wakati wa mjerumani na mpaka leo hutumika kusaga nafaka eneo la mto zigi Amani? Je wajua kuwa kuna maua na miti pamoja na ndege ambao duniani kote hakuna wanapatikana Amani tu katika Mkoa wa Tanga?

Mwisho kabisa niseme kuwa hakuna mji unaokuwa kiutalii kama haujatangazwa na wenye mji husika na pia kama mazingira asilia yaliyopo hayajaekewa miundombinu ya kuufanya utalii ufanyike kwa kiwango cha hali ya juu.

Amarison Consultancy imedhamiria kuandaa vipindi vya TV kwa jili ya kuutangaza utalii wa Tanga na kila wilaya itatangazwa na kufamika vivutio vyake vya utalii tunaendelea kutengeneza vipindi vyetu wakati ukifika tutahitaji udhamini wa kuvirusha hewani kwenye TV  yoyote ile baada ya kutimiza vigezo na masharti.


              




Friday 23 September 2016

TANZANIA YASHINDA KESI DHIDI YA IPTL

Uamuzi wa ICSID kuhusu IPTL mshindi Ni Tanzania

Septemba 12, 2016 Mahakama ya Usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji iliwasilisha rasmi maamuzi yake Kwa pande zilizokuwa kwenye mgogoro kuhusu mradi wa kufua umeme Nchini, IPTL. Mahakama hiyo iliamuru kwamba Benki ya Standard Chartered ya Hongo Kong ( SCB-HK ) ilipwe dola za Kimarekani 148 milioni sawa na Fedha za Kitanzania shilingi 320 bilioni. Mahakama hiyo Pia imeamuru kuwa kuchotwa Kwa Fedha kutoka akaunti maalumu ya TEGETA Escrow hakukuondoa Haki ya ya Benki ya SCB-HK kwenye kampuni ya IPTL na hivyo kisheria kwamba Benki hiyo Kwa sasa ndio mwenye uhalali wa shughuli zote za IPTL.

Ilinichukua Siku takribani 2 kusoma na kusoma tena tuzo hii (Award ) ili kuweza kuielewa haswa maana yake Kwa Nchi yetu. Ikumbukwe kwamba niliongoza Kamati ya Bunge iliyoagiza uchunguzi wa sakata la TEGETA Escrow Account na kuandaa Taarifa Maalumu ya Kamati ya PAC iliyosomwa na kukubaliwa rasmi na Bunge na kupitisha maazimio 8 yaliyopaswa kutekelezwa na Serikali. Baada ya kuisoma Kwa kina Tuzo hiyo ya ICSID nilichoona Ni kwamba masuala Yale Yale ambayo PAC iliyafafanua Bungeni Mwezi Novemba mwaka 2014 ndio hayo hayo yaliyopelekea tuzo hiyo. Kwa maana hiyo Ni kwamba iwapo Serikali ingetekeleza Maazimio ya Bunge yote Leo hii tungekuwa kwenye nafasi nzuri sana ya kulimaliza suala Hilo kabisa na kuachana kabisa na mgogoro huu ambao unanyonya Fedha za Watanzania.

Kuna masuala makuu 2 ambayo yakieleweka suala la kashfa ya IPTL litakuwa limeeleweka na maamuzi yanaweza kufanyika kumalizana nalo.

1. baada ya mbia ya kampuni ya Mechmar kufilisika nchini Malaysia, Ni Nani mwenye Haki na Mali za IPTL?
2. Tozo ya malipo ya umeme uliozalishwa na IPTL ilizidishwa?
Kwenye Taarifa ya Kamati ya PAC tulionyesha Kwa vielelezo na ushahidi kwamba kampuni ya PAP haikuwa ina umiliki wa kihalali wa asilimia 70 ya Hisa za IPTL. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alionyesha dhahiri kuwa vyeti vya Hisa ( shares certificates ) za kampuni ya Mechmar kwenye IPTL walikuwa nazo Benki ya SCB-HK Kama dhamana ya mkopo waliowapa IPTL. CAG aliziona hati hizo Kwa macho yake kwenye uchunguzi wake ambao ndio uliotumika na PAC kufikia maazimio 8 ya Bunge.

Vile vile Kamati ya PAC ilionyesha Kwa ushahidi kuwa PAP hawakufuata sheria za Tanzania katika kumiliki IPTL ikiwemo kwamba walikwepa kodi kupitia kampuni iliyoitwa PiperLink ya British Virgin Island. TRA walikiri mbele ya Kamati kuwa wakati Mahakama Kuu inatamka kuwa PAP wapewe ' masuala ( affairs ) ya IPTL ) hawakuwa na uhalali wa kufanya Biashara Tanzania kwani hawakuwa wamepewa kibali na Kamishna Mkuu wa Kodi cha kuthibitisha utwaaji wao wa kampuni ya IPTL. Hivyo Kamati ililiambia Bunge kuwa PAP ni matapeli wa Kimataifa waliopiga ganzi Mfumo wa Serikali ya Tanzania Kwa kutumia rushwa na hivyo kuhalalishiwa umiliki wa IPTL ili kuchota Fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya TEGETA Escrow Benki Kuu ya Tanzania.

Hata Gavana wa Benki Kuu alipowaomba PAP uhalali wa wao kumiliki IPTL walichotoa ni kitu kinachoitwa Deed of Assignment badala ya shares certificates. Watanzania watakumbuka kuwa Deed of Assignments ndizo zilizotumika kuiba Benki Kuu kwenye wizi wa EPA mwaka 2004-2005. Jambo la kushangaza Ni kwamba karatasi hiyo ya kugushi ilikubaliwa na hivyo Bwana Harbinder Singh Seth wa PAP akaruhusiwa kuchota mabilioni ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania. Kwa mujibu wa Mwanasheria wa TANESCO Bwana Richard Rweyongeza TANESCO waliilipa PAP $245m Sawa na shilingi 530 bilioni. Itakumbukwa kuwa wakati PAC inasoma Taarifa yake Fedha hizo zilikuwa tshs 306 bilioni tu.

Katika tuzo yake ICSID imethibitisha kuwa PAP hakuwa mmiliki wa IPTL na hivyo alilipwa Fedha za TEGETA Escrow kimakosa. Hoja hii imethibitisha Hoja ya PAC na Bunge la Tanzania ambayo ilipingwa vikali na Serikali ya wakati huo ambayo iligeuka mtetezi wa PAP. Uamuzi wa ICSID kwamba TANESCO wailipe SCB-HK unathibitisha kuwa PAP alipewa Fedha za TEGETA escrow kitapeli.

Baada ya kumaliza hoja hiyo twende Hoja ya pili; je Hata Kama PAP wangekuwa Ni Wamiliki halali wa IPTL walilipwa ziada?

Itakumbukwa kwamba PAC ililiambia Bunge kuwa mgawo wa Fedha ulipaswa kusubiri kukokotoa kanuni za mgawo ambazo ziliamriwa na Mahakama hiyo ya ICSID. Hoja kubwa ya PAC ilikuwa ' Ni Kwanini tulifanya haraka kutoa Fedha kabla ya Uamuzi wa kiwango gani kilipwe? '. Hoja hii ndio iliyochagiza kuwa mule ndani ya TEGETA escrow kulikuwa na Fedha za umma. Uamuzi wa kukokotoa ukatolewa Mwezi Februari mwaka 2014 lakini katika mjadala mzima wa sakata la TEGETA escrow Serikali ilikataa kata kata kutekeleza Uamuzi huu. Hata kwenye Hoja za TANESCO mahakamani huko hawakuwa kabisa na Hoja kulinda Uamuzi ule. Hata hivyo ICSID imeamua kuwa tulikuwa tunaliwa Kwa kulipa tozo kubwa zaidi ya kiwango tulichopaswa kulipwa. Hii maana yake Ni kwamba Hata kwenye hizo za wizi tuliilipa PAP zaidi ya tulichopaswa kuwalipa.
Katika magazeti ya Leo wakili aliyeiwakilisha TANESCO anasema " tulibishania Hoja ya kulipa Kwa viwango vya zamani ikaamuriwa hesabu zifanyike upya Mahakama iliamuru hesabu zifanyike upya Kwa kutumia mkopo wa wana Hisa ". Hii ndio Hoja ambayo PAC iliijenga Kwa muda mrefu na kubezwa na Serikali ndani ya Bunge Kwa mbwembwe zote. Wakili wa TANESCO anaendelea " kutokana na hesabu hizo gharama ilikuwa chini. IPTL ililipwa zaidi hivyo inatakiwa kurejesha Dola za Marekani zaidi ya milioni 100 Kwa TANESCO ".

Hii ndio ilikuwa Hoja ya PAC ambayo ilitokana na maagizo ya CAG kwamba TANESCO wakae chini na SCB-HK kupiga hesabu upya. Hoja hii ilikataliwa na Serikali na TANESCO wenyewe ilipotolewa na PAC lakini Leo mwanasheria wa TANESCO aliyeiwakilisha TANESCO katika Mahakama ya Usuluhishi ya ICSID anakiri tuliwalipa zaidi IPTL.

Jambo la kushangaza Ni kwamba, licha ya ushindi huu mkubwa Kwa Tanzania na TANESCO wanasheria wanataka tukate rufaa. Magazeti ya Serikali ya Dailynews na habari leo ndio yameongoza na habari hiyo. Ikumbukwe kuwa magazeti hayo ndio Siku zote yamekuwa yakiitetea pap na Bwana Seth. Ni dhahiri kuwa ama wanasheria wanataka waendelee kulipwa Fedha kwenye kesi au kuna shinikizo kubwa kutoka Kwa wanaofadika na mchezo huu wa kutapeli ili waendelee kufisadi Nchi. Uamuzi huu wa ICSID unatuweka kwenye nafasi nzuri sana ya kulimaliza kabisa suala la IPTL kwani umetuonyesha kuwa;
1)Kwa miaka yote ya uwepo wa IPTL tumekuwa tunapigwa Kwa kulipa capacity charges Mara mbili ya kiwango tulichopaswa kulipa
2)Tulitapeliwa na Bwana Seth kupitia kampuni ya PAP ambayo Wamiliki wake wengine 50% mpaka sasa hawajulikani Ni kina Nani licha ya kuwajua Kwa jina la Simba Trusts ya Australia.  

Wakati wanasheria na baadhi ya maofisa wa Serikali waliofadika na mgawo wa TEGETA escrow wanataka kukata rufaa wanajua kuwa maamuzi ya ICSID hayana rufaa Kwa mujibu wa Ibara ya 53 ya mkataba wa ICSID ( no appeal except those provided for in the ICSID Convention ). Hadhi  yake Ni Sawa na maamuzi ya Mahakama ya juu kabisa ya Tanzania Kwa mujibu wa Ibara ya 54 ya mkataba wa ICSID ( convention ). Hata hivyo maamuzi hayo yanaweza kuombewa kufutwa Kwa kutumia Ibara ya 52(2) Kwa sababu maalumu ambazo Ni

a). Baraza la Usuluhishi halikuundwa kisheria ( properly constituted ). Ijulikane kuwa Baraza hili huteuliwa na washiriki wa kesi. SCB-HK waliteua msuluhishi wao, TANESCO waliteua wao na Kwa pamoja wakateua Rais wa Baraza. Hivyo TANESCO hawana Hoja maana Hata msuluhishi waliteua wao kakubaliana na maamuzi haya ya tuzo hii.
b). Kwamba Baraza lilienda nje ya mamlaka yake. TANESCO walishiriki mwanzo mwisho na hawakuwa na malalamiko kuhusu Hilo wanawezaje kuwa na malalamiko sasa. Hata msuluhishi wao kakubali maamuzi haya.
c). Kwamba kulikuwa na rushwa kwenye kufikia maamuzi haya. TANESCO wanaweza kutoa ushahidi Kama Hata msuluhishi waliyemteua wao alihongwa!
d) kwamba tuzo haina sababu za kufikia maamuzi haya. Kwa walioisoma tuzo hii wanajua kuwa sababu zipo kinagaubaga kabisa.

Kwa maoni yangu kutaka kesi iendelee Ni kutaka kulinda maslahi ya wanaofadika na suala zima la IPTL. Suala hili sasa liishe. Nchi imeshaliwa sana. Itoshe.

Ushauri wangu Kwa Serikali Ni Kama ifuatavyo

1. Kutekeleza tuzo hii ya ICSID bila kusita
2. Kuiamrisha kampuni ya PAP kurejesha Fedha zote za ziada ilizolipwa kutoka akaunti ya TEGETA escrow. Kwa mujibu wa tuzo hii Ni jumla ya tshs 202 bilioni
3. Kuitaka kampuni ya PAP kuilipa Benki ya SCB-HK kutokana na hati iliyowasilisha Benki Kuu kwamba madai yeyote yakitokea katika IPTL PAP ndio watalipa ( indemnity ).
4. Kuchunguza na kuishtaki PAP na Bwana Harbinder Singh Seth Kwa utapeli na utakatishaji wa Fedha Kwa mujibu wa sheria za Tanzania
5. Kuchunguza na kuwashitaki maofisa wote wa Serikali walioshirikiana na Seth kuchota Fedha Benki Kuu
6. Kuilipisha faini Benki ya StanBic Tanzania Kwa kushiriki kwenye vitendo vya kutakatisha Fedha kufuatia miamala ya TEGETA escrow
7. Kufunga kabisa suala la IPTL Kwa kuvunja mkataba na kuitwaa mitambo Kwa mujibu wa sheria za Tanzania

Natumai kuwa watu wenye nafasi za Uongozi wa umma ambao maamuzi Yao yamefikisha Nchi hapa watachutama na kuondoka katika Uongozi wa umma. Tumefikishwa hapa na wizi na tamaa za watu madalali wa matapeli. Ninaamini kuwa Rais John Pombe Magufuli hatakubali Nchi hii kuendelea kupigwa na matapeli.

Zitto Kabwe, Mb
Kigoma Mjini