Thursday 20 October 2016

MIKOPO ELIMU YA JUU

Nawashangaa watanzania

MTU anasomesha mtoto ada milioni 3

Analalamika kukosa mkopo wa 1.5 m kulipia ada ya chuo kwa MWAKA

Watu wanailaumu serikali eti wanafunzi wamekosa mikopo bali hawalaumu waliokopeshwa kuingia mitini kutokulipa

Wanasingizia hawana ajira wakati kuna kujiajiri na kwa mwezi unatakiwa kulipa kima cha 50000 kwenda juu hiki ni kiwango nilichokuwa nikilipa deni langu la bodi ya mikopo sijui sasa kima cha chini ni kiasi gani.

Hukusoma ili uajiriwe umesoma ili uondoe ujinga na upumbavu hatimaye ujiajiri.  uendeshe maisha yako na ulipe deni la mkopo wa elimu ya juu.

Ni ujinga wa hali ya juu kusema wanafunzi 66000 wa elimu ya juu wamekosa mikopo

Wakati kuna vijana zaidi ya milioni toka 1994 mpaka 2015 hawajalipa hata shilingi wanadaiwa .

ILI WATANZANIA WENGINE WAWEZE KUKOPESHWA KUSOMA ELIMU YA JUU

WEWE ULIYEMALIZA MWAKA 1994 HADI 2015 LIPA ILI WENGINE WAKOPESHWE.

Kwanza jamii yetu ishajitenga siku nyingi eti wanaosoma shule za serikali ni masikini na wanaosoma shule za kulipia ni matajiri.

Katika msingi huu wanaomaliza Shule za serikali nashauri wapewe kipaumbele kwenye mikopo maana hawana uwezo.

Serikali na bodi ya mikopo nashauri kigezo kimojawapo cha kupata mkopo wa elimu ya juu iwe ni kuangalia anayeomba amehitimu elimu Yake Wapi

Shule ya msingi

Shule ya sekondari

Kidato cha sita

Maaana kuna wanaolipa milioni 4 kusomesha  chekechea eti na wao wapewe mikopo kwa kuwa wana watoto elimu ya juu alaaaa

Dahh ningekuwa nina mamlaka ya mwisho

Ningehakikisha aliyesoma Shule ya msingi ya serikali la kwanza hadi la saba pamoja na sekondari ya serikali na kidato cha sita kahitimu Shule ya serikali hakika huyu angepata mkopo 100%

Hapa hakuna ubaguzi maana wakati wewe unasoma Shule ya mamilioni na mwingine anasoma shule ya elimu bure hukuuona huo ubaguzi ndio uje kuuona chuo kikuu kwa kuwa umekosa mkopo?

Kama uliweza kulipa malaki na mamilioni kuanzia shule ya msingi endeleaaa tu baba kulipa mamilioni elimu ya juu iweje ule ng'ombe mzima uahindwe mkia?

Kama kuna aliyesoma kwa ada ya chini ya laki moja elimu ya msingi mpaka kidato cha sita aendelee tu kusaidiwa na serikali kukopeshwa na kupata elimu ya juu maana huyu ndio hana uwezo.

KILA MBUZI ATAKULA KWA UREFU WA KAMBA YAKE.

Amarison
2016

No comments:

Post a Comment