HONGERA MH JAKAYA KIKWETE
Rais mstaafu Dk JM Kikwete ametunukiwa Tuzo Maarufu ijulikanayo kama SPEAKUP AFRICA. Tuzo hii hutolewa kwa watu maarufu na mashuhuri ambao wamethibitika kutoa mchango katika bara la Afrika.
Miongoni mwa viongozi wa Afrika waliotunukiwa Tuzo hiyo ni pamoja na Waziri wa afya na masuala ya kijamii wa Senegal, Prof Awa Mariel Coll-seck.
Hafla hii ya kuwatunuku Tuzo hiyo imefanyika 22 Sep 2016, katika ukumbi wa American Museum of Natural History, New York, nchini Marekani.
Hongera JK, Hongera CCM, Hongera Tanzania kwa kuendelea Kutambuliwa na Ulimwengu kwa Mchango wenu katika Jamii
Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Magoiga SN-Mwanza
Mwenyekiti wa Muda-CCM Tawi la Mitandaoni
No comments:
Post a Comment