Thursday 22 September 2016

USIONE UKADHANI ATCL IMETOKA MBALI

KAMA HUJUI SEMA SIJUI UFAHAMISHWE SIO KUPINGA KILA JAMBO

NAIPONGEZA SERIKALI KWA KULIFUFUA SHIRIKA LA NDEGE LA ATCL NA HUU NI MWANZO MZURI.

Kundi kubwa sana la vijana waliopo vyuoni wengi wamezaliwa miaka ya 1990 na kuendelea ,  yaani wakati wanazaliwa ni miaka miwili ndio nchi ya Tanzania inakubali kuwa na siasa za upinzani hivyo hawakuona utawala wa Mwl Nyerere Mzee Mwinyi wengi wamebaleghe utawala ukiwa ni wa mzee Mkapa kwa hiyo wanamengi ambayo hawayajui kuhusu Tanzania.

Kuna haja kubwa sana ya vijana kujengewa uwezo wa kuifahamu historia ya uchumi ya mashirika mbalimbali ndani ya Tanzania maana wanapoona shirika likifufuliwa au kama lilipoteza muelekeo basi huanza kupinga na kudharau jitihada za serikali.

Wamelishwa propaganda za kudharau kila jambo jema la serikali katika jitihada na harakati za kufufua sekta mbalimbali za uchumi wa Taifa hili.

Hapo awali tulikuwa na shirika la ndege tangu wakati wa Mwl Nyerere MZEE mwinyi na lilikuwa likifanya kazi vizuri uwezo wa shirika uliingia kipindi kigumu baada ya kufa JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI.

Ufuatao ni muhtasari wa kuyumba na kulifufua au kulipa uhai shirika hili ili liweze kuwa sehemu mojawapo ya chanzo cha mapato ya Taifa letu.

Kwa kifupi nchi yetu ilianza kusimama pekee kwenye shughuli za anga baada ya kuvunjika iliyokuwa jumuiya ya Afrika Mashariki 1977.

Hii jumuiya ndiyo iliyokuwa inamiliki kwa pamoja  Shirika la Ndege la Afrika Mashariki yaani East African Airways EAA.

EAA ilikuwa na makao yake makuu Jiji la Nairobi Kenya na hivyo miundombinu yote muhimu ya uendeshaji ilikuwa huko na hata wafanyakazi wengine kutoka ndani ya nchi wanachama walikuwa wakiishi Nairobi.

Baada ya kuvunjika ghafla kwa EAC, Kenya ilizuia ndege  zote isipokuwa nadhani ndege mbili au moja ambayo ilikuwa Kwenye Anga ya Tanzania wakati inatangazwa jumuiya imevunjika.

Ndege hiyo ilikuwa Fokker Friendship F-27.
Kimsingi Tanzania tulijikuta tunaamka asubuhi hatuna huduma ya usafiri wa Anga.
 haraka Rais Nyerere alimteua Jaji wa Mahakama Kuu Mh Yahya Rubama kuongoza kikosi kazi cha kuanzisha ATC na kuweza kupata ndege kadhaa ndani ya muda mfupi.

Kazi ilikuwa ngumu sana. Ndege hizo zilipatikana kwa njia ya mkopo na serikali wakati ikiendelea kuimarisha mtaji wa ATC mwaka1978 tukaingia kwenye vita na Uganda hali ambayo iliteteresha uchumi wa nchi yetu lakini ndege za ATC zilitoa mchango mkubwa wakati wa vita.

Baada ya vita hali ya uchumi iliendelea kuwa ngumu kwa waliokuwepo watakumbuka ugali wa Yanga, uhaba wa bidhaa nk. Hivyo basi ATC nayo ilipitia wakati mgumu sana kimtaji na pia kiuendeshaji.

 Lakini bado tuliweza kuhhimili na kuendeleza sekta ya anga na ATC ikiwa Ni mhimili mkubwa kwa kutoa huduma na mafunzo katika nyanja mbalimbali ikiwemo marubani, mafundi, nk

Miaka kadhaa baadae, wakati nchi yetu ikiendelea na jitihada za kufufua uchumi, Bank ya Dunia na Shirika la Fedha duniani vilisimamia urekebishaji wa sera zetu na kutaka serikali ijiondoe kwenye kufanya biashara na badala yake ijikite kwenye kukusanya kodi, biashara iachiwe sekta binafsi. Sera hii ya benki ya dunia na shirika la fedha duniani walikuja na mpango uitwao Structural Adjustment Program mpango huu ndio ulioshinikizwa sana na mataifa ya magharibi kuwa lazima utekelezwe

Hapa ndio mwanzo wa kufa kila kilicho cha serikali.

Hapo ndiyo mwanzo wa sera ya taifa ya ubinafsishaji iliponza na kutakiwa kuyabinafsisha mashirika ya umma.
Mashirika kadhaa yaliwekwa sokoni ikiwemo ATC.

Mashirika kadhaa yaliwekwa sokoni ikiwemo ATC chini ya usimamizi wa Tume ya Rais ya Urekebishaji wa Mashirika ya Umma yaani PSRC na hapo shughuli zote za Standing Committee  on Parastatal Organizations (SCOPO) ilikoma kufanya kazi.

Pamoja na mambo mengine, shirika litakalo kuwa specified kwa ubinafsishwaji likiwekewa masharti maalum kwa mfano

 ATC katika kipindi chote likisubiria ubia na halikutakiwa kufanya  single investment inayozidi USD 1Million. Kwa sekta ya anga uwekezaji wa USD 1m Ni mdogo sana na ATC ilikuwa kwenye kipindi hicho cha kusubiri ubia kwa muda mrefu sana na haikuweza kupata ubia hadi inavunjwa mwaka 2002.

Matokeo yake nini, ni kwamba mtaji wa ATC uliendelea kudumaa na kusababisha iendelee kupata hasara zaidi na zaidi.

Mwaka 2002 serikali ilisitisha ATC ambayo ilianzishwa 1977 kwa sheria ya Bunge ambayo haikuwa inaruhusu umiliki wa pamoja na sekta binafsi na hivyo kuanzisha Kampuni ya Ndege ya Tanzania yaani Air Tanzania Company Limited kwa kutumia sheria ya makampuni yaani Company Ordinance Chapter 212.

 ATCL baadae iliuza 49% ya hisa zake kwa South African Airways December 2002. Baada ya hapo SAA walipewa jukumu la kuendesha menejimenti ya ATCL lakini kutokana na mgongano wa kimaslahi ATCL ilidhoofishwa na kufikia maamuzi ya serikali ya kuzinunua tena hisa 49% na kuiweka katika umiliki wa 100%.

Hivyo basi unazoziona sasa Ni juhudi za kulifufua shirika hilo Nadhani hatutakiwi kuzibeza bali kuunga mkono.

Muda ni mwalimu wetu mzuri, hutufundisha mengi mazuri na kututaka kuendana nayo.

Nyakati zimebadilika sana hasa kwenye biashara ya usafiri wa anga. 1977 ATC inaanzishwa hakukuwepo na Emirates wala Etihad au Qatar Airways. Haya mashirika matatu ni makubwa sana kiasi cha kuweza kuyaweka kwenye wakati mgumu kibiashara mashirika makubwa na kongwe kama British Airways, Sabena, Alitalia, Lufthansa, KLM, Air France, Swiss Air nk.

 Baadhi ya mashirika ya ndege yamefutika na mengine yamejipunguza. Kwa mfano mashirika kongwe yanayokuwa Dar sasa hivi KLM na Swiss nadhani mengine yameshindwa ushindani.
Pili, Nairobi ni saa moja tu kutoka Dar na ni kitovu kikuu cha usafiri wa anga hapa Africa Mashariki hivyo basi operators wengi wa safari ndefu wanaamua kuishia Nairobi zaidi maana yake Nairobi ina wasaa mkubwa kulinganisha na Dar.

Hivyo basi unapotaka kuanza safari za mbali lazima uingie kwenye hasara.

Tanzania yaani nchi yetu ina safari za ndani nyingi sana kuliko nchi nyingine  kusini mwa Africa ukiitoa South Africa. Hivyo basi hizi safari za ndani  Ni fursa, ni soko ambalo hatuna ushindani na mashirika ya nje, tuna uwezo wa kulijenga na kuliendeleza tunavyotaka.

Serikali kwa kuliona hilo imeendelea na uimarishaji wa viwanja vya ndege nchi nzima, kutoka Pemba hadi Sumbawanga, kutoka Bukoba hadi Mtwara. Ili kulikamata soko hili la ndani Ni lazima uwe na zana zitakazoweza kuhudumu viwanja vingi zaidi, Q400 Ni jawabu.

Wakati wa ATC zilikuwepo DHC Twin Otter kwa ajili ya viwanja kama Sumbawanga Nachingwea, Kilwa, Mafia, Iringa, Pemba, Bukoba, nk
F27 ilikuwa ikihudumu baadhi ya hivyo viwanja pamoja na viwanja vingine kama Zanzibar, Tanga, Mtwara, Lindi, Dodoma, Tabora, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Musoma, Kia, Kigali, Bujumbura, Mombasa, nk

B737 ilihudumu Zaidi Kia Mwanza, Zanzibar, Mtwara, Johannesburg, Lusaka, Lilongwe, Nairobi , Entebbe, Iilongwe, Dubai, Muscat, Aden,

Tuiunge mkono serikali kwa kuhakikisha shirika hili linafanya kazi kwa ufanisi.

Mwandishi

Isaac Kitogo

Imekusanywa na kufanyiwa majumuisho na

 Amarison Tanga Tanzania

No comments:

Post a Comment